Saturday, January 23, 2010

WALIOWENGI WANASEMA KUWA MTI UKIWA MKAVU UNA NINI..............?


HAPA! KAZI KAKA
Kwa kila jambo lilolo jema huwa na magumu sasa jiandae kuwa na maema pia ukutane na yaliyo magum karibu katika mwak huu Sijui dada yangu aliyoko Norway yupo maana amekaa kimya sana kama kwao walivyokaa sana kimya kule kunako na dagaa wazuri yaani ziwa Nyasa He! naomba ujitokeze we mama.


Haya ni majadiliano ya Nini Wadau? maana kulia ni Kocha Mkuu wa SimbaPatrick Phiri na katikakati ni Mh.Waziri wa kazi na Maendeleo ya Vijana Juma Kapuya na wa mwisho ni mkereketwa wa Simba wakimsikiliza akimwaga porojo

Mshambuliaji wa timu ya Simba Mussa Hassan 'Mgosi' akitafuta mbinu za kumtoka beki wa timu ya Prisons ya Mbeya jana Laurian Mpalile katika mchezo wa jana uliofanyika katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam.Mchezo huo ulimalizika kwa Simba kuibuka na ushindi wa mabao 3-1


"Nashukuru umekuwa kocha pekee ulioonyesha uwezo wa kufundisha hapa nchini kwa kweli mimi naipenda sana Simba hasa hivi unavyoshinda kila mchezo tena umeweka historia ya pekee itabidi nikae nikufikirie nikupe jimbo" Hivi ndivyo inavyoonekana akisema Waziri wa Kazi na maendeleo ya Vijana Juma Athuman Kapuya jana wakati Simba ilipokuwa ikicheza na Prisons ya Mbeya ambapo Simba iliibuka na ushindi wa mabao 3-1.

hizi zilikuwa za jana wakti Simba ilipotoa kipigo kwa Prisons ya Mbeya

Wadau wa soka wakijadiliana jana katika mchezo wa Simba na Prisons ya Mbeya ambapo Simba waliibuka na ushindi wa mabao 3-1 Mdau Mkuu anayeamini anaipenda Simba Mh.Juma Kapuya akilonga na jamaa ambye jina lake halikufahamika .

watoto eeehe! mzunguko huo!

Watoto wa shule ya awali ya Galomba iliyopo Keko Michungwani Dar es Salaam, wakiwa katika mchezo. Michezo kama hii kwa watoto ni muhimu kwa ajili ya kujenga afya zao na kuwajenga kiakili zaidi.

Pole Essien wa Taswa..

Kutokana na beki mahiri wa timu ya Taswa Fc Ernest Mbozi kuvunjia mguu wakati akiwa katika mechi ya kirafiki na timu yake ya Chuo, sasa atakuwa nje kwa muda usiopungua wiki 6.

Friday, May 22, 2009

unaweza nyoni

ERASTO NYONI EDWARD:

Beki Stars anayetamani safari yake ya nje ianzie Rwanda

na said makala

NI miongoni mwa wachezaji chipukizi wa mwanzo mwanzo kuitwa tokea mikoba ya kuinoa timu ya soka ya taifa, Taifa Stars iwe mikononi mwa Mbrazil, Marcio Maximo.
Alipoitwa kwa mara ya kwanza mwaka juzi akiwa na Vital’o ya Burundi, hakuwa mchezaji anayefahamika sana nchini licha ya ukweli kuwa aliwahi kuichezea AFC ya Arusha iliyoshiriki ligi kuu ya Vodacom, msimu wa 2005.
Lakini bao lake lililoipatia ushindi Taifa Stars dhidi ya Burkina Faso wakati wa kusaka nafasi ya kufuzu kwa kombe la Mataifa ya Afrika, 2008 alilofunga ugenini jijini Ouagadougou, ndilo hasa lilimjengea jina kubwa nchini Tanzania.
Kwa sasa, Nyoni ambaye ni mzaliwa wa Songea mkoani Ruvuma ni mchezaji wa kikosi cha Azam FC kilichokuwa chini ya Mbrazil, Neider Dos Santos na msaidizi wake, mzawa Sylvester Mash, akiwa na mkataba wa mwaka mmoja unaomalizika Agosti mwaka huu.
Mara nyingi amekuwa akicheza kama mlinzi wa kati au pembeni kushoto, lakini katika mazoezi ya Taifa Stars yanayoendelea hivi sasa ikijiandaa kwa mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya New Zealand, Nyoni anachezeshwa kama beki wa kulia, nafasi ambayo inamilikiwa na Shadrack Nsajigwa katika kikosi hicho.
Akiwa amezaliwa Julai 7, 1983 (Sabasaba), alipata elimu yake ya msingi katika shule ya Mahenge iliyopo mjini Songea kuanzia mwaka 1993 hadi alipomaliza 2000. Kutokana na matatizo mbalimbali, hakufanikiwa kuendelea na elimu ya Sekondari.
Kama ilivyo kwa wanasoka wengi, alianza kupenda soka akiwa na umri mdogo lakini hasa aliweza kuibuka pale alipochaguliwa katika timu ya shule katika michezo ya UMISHUMTA, akiwa darasa la nne.
Kufuatia kuonyesha kipaji cha juu katika michezo hiyo, Nyoni aliweza kuwavutia mashabiki wengi na kaka yake, anayemtaja kwa jina la George, aliahidi kumpeleka katika timu aliyokuwa akiichezea, iliyoitwa Five Star.
“Kweli nilioneka ni mtoto mdogo lakini niliweza kucheza vizuri. Na kweli alinipeleka lakini kutokana na umri wangu kuwa bado mdogo, nilikuwa sichezi mechi zaidi ya kufanya mazoezi na wakubwa,” anasema Nyoni.
Alipomaliza darasa la saba, ndipo akajiunga rasmi na timu hiyo na kukaa nayo kwa muda wa mwaka mmoja, akicheza ligi ndogo ndogo zilizokuwa zikiandaliwa na watu mbalimbali kwa zawadi za fedha.
Ni ligi hizo ndizo zilizomweka katika kiwango kizuri kwani siku moja, kaka yake aliyekuwa akiishi Arusha wakati huo, alimtumia ujumbe kumtaka kwenda mkoani humo akajaribu bahati yake katika mashindano yaliyoandaliwa na shule ya vipaji ya Rolling stone Football Academy.
Mashindano hayo yalishirikisha wachezaji chipukizi kutoka nchi za Burundi, Kenya, Zanzibar na vyuo mbalimbali.
Alifurahia wito huo na kuamini kuwa wakati wa kutimiza ndoto zake za kusakata kandanda kwa kiwango kikubwa ulikuwa umewadia.
Na ikawa kweli kwani alionyesha uwezo mkubwa wa kucheza soka na kuisaidia timu yake ya Rolling stone kuibuka mabingwa, hali iliyopelekea kupata nafasi ya kusajiliwa na AFC.
Alikuwa ni kocha wa AFC wakati huo ikishiriki ligi kuu, Hali Mtumwa ndiye aliyemdokeza nia yake ya kumtaka aichezee timu yake, jambo ambalo alilikubali mara moja.
Mwaka mmoja baadaye, viongozi wa soka wa Burundi, ambao waliwahi kumuona kwenye mashindano yale ya vipaji, walimfuata na kumweleza lengo lao la kumtaka kuelekea nchini humo kwa ajili ya kucheza soka.
Kocha wake Mtumwa, hakuwa na kinyongo kwani alimruhusu na hivyo kumfanya Nyoni kuvuka mpaka hadi Burundi alikojiunga na Vital’o.
Katika safari hiyo, aliandamana na mtoto wa kocha huyo, Abdalah Hali ambao wote walisajiliwa na miamba hiyo ya Burundi.
“Majaribio yalienda vizuri, nilikubalika na tukatiliana mkataba wa miaka miwili na nusu ambapo katika miaka hiyo ya 2006 na 2007 niliweza kuisaidia timu hiyo kuwa mabingwa mara mbili mfululizo,”
“Msimu wa 2008 ulipoanza nilicheza nusu tu, nikaondoka na kuja kujiunga na Azam ambayo nimesaini nayo mkataba wa mwaka mmoja unaomalizika Agosti mwaka huu,” anasema Nyoni.
Moja ya sababu kubwa iliyomrejesha nyumbani, ni kutaka kwake kuonekana ili aendelee kuitwa kikosi cha Stars, ingawa pia upinzani wa ligi kuu ya Vodacom umechangia.
“Wazo la kucheza nje lipo lakini sio kwenda katika nchi kubwa kisoka, nataka nianzie karibu ili kujiweka fiti kwanza na nchi ya kwanza ni Rwanda maana wananitaka sana kwani nilishawahi kufanya mazungumzo nao na waliridhia kauli yangu ya malipo hivyo natarajia mkataba wangu ukimalizika na Azam nitaenda kujaribu bahati yangu,”anasema.
Akiwa kikosi cha Vital’o, alicheza pamoja na wachezaji kadhaa Watanzania, ambao ni pamoja na Abdalah Hali, Abdalah King’alu, Stainless Minzi na Hafivi Mussa, ambao hata hivyo, kwa sasa wote wamerejea nyumbani.
Kuhusu mchezaji wa nyumbani anayemvutia, mchezaji huyo anasema kwa kujiamini.
“Hakuna kama Haruna Moshi ‘Boban’. Anaweza mpira, ana kipaji chake cha kipekee na ananivutia sana, kama ananisikia kaka yangu huyo ajaribu kutulia, anaweza sana, pia ajaribu soka Ulaya anaweza kufuzu bila vipingamizi kwani uwezo wake ni wa kiwango kikubwa,”anasema.
Anasema wakati kiungo huyo mahiri alipokuwa Stars kabla ya kutemwa alikuwa mfano mkubwa kwake, kwani anapokuwa uwanjani huonyesha kilichompeleka na anakiri kumuiga kiungo huyo nyota wa Simba kiuchezaji.
Kwa nje, Nyoni anavutiwa na kiungo wa Barcelona ya Hispania, Andreas Iniesta pamoja na Xavi Hernandez na kusema ni wachezaji wenye kiwango cha juu kuliko hata Ronaldo.
Anasifu ushirikiano kati ya Iniesta na Lionel Messi wawapo uwanjani kwani mmojawapo asipokuwepo, mwenzake huonekana kuwa na huzuni.
Si soka pekee linalomkuna beki huyu bali anavutiwa pia na muziki wa kizazi kipya, hasa mzee wa Commercial, Ambwene Yessaya ‘AY’.
Huyu ndiye Erasto Nyoni Edward, beki ambaye Maximo anamwandaa kwa ajili ya kuiua New Zealand mwezi ujao.

Friday, March 20, 2009

siamini hivi kweli au unaweza


Huwezi kusikitika ukibahatika kumwona huyu dada kwani anaweza kuwa wa kwanza kwa uwezo wa kucheza muziki akiwa jukwaani hasa katika kuzungusha kiuno kwa ustadi mkubwa. fikiria kuhusu mako huu haloooo!

Sunday, March 15, 2009

sawa


hizi ndizo hazina ambazo watanzania wamejiwekea nchini watalii mbalimbali wamekuwa wakifika na kuingiza kipata kupitia mali hizi za mikono Tanzania inapendwa na wengi huyu ni mhuzi wa vinyago kama alivyokutwa na blog yetu.

xc

hizi zipo

kazi hizi za filamu


Wakati Jumba la dhahabu liliwakamata wapenzi wa Tamthiliya niliwahi kjiuliza wasanii hawa wenye ubunifu mkubwa hivi kama mzee Chilo,Frank,Jini Kabula,Mama mtei na wengine wanatokea wapi? wengine walinijibu wanatokea Nyasa kule kwa kina Yasinta nikamkubuka sana Yasinta kwa sababu ni mmoja wa watu ambao kila siku wanatembelea blog yangu lakini bwana hawa wanaweza kazi hongera Mkoa husika kwa kutoa vjana hodari hebu ona hapa wasanii waliotoka na Filamu ya hosteli ambayo inatamba hivi sasa

haya gerd

walikuwa na kazi hawa


mechi ya jana dhid ya liverpool ilivyofaana wababe hawa wanapokutana huwa hapakali katika jiji la Dar es Salaam kwani mashabiki kibao hukaa katika vijiwe vyao wakidadisi juu ya timu ipi bora kuliko nyingine hasa Arsenal,Man U,na Liver pool kama sio ile nyingine ya The Blues 'Chelsea.

Saturday, March 14, 2009

ya magufuli ni ya kweli

Alikaa kimya midhili ya tembo aliyeingiwa na sisimizi puani,hakuwa na papara na kazi zake hili ni jambo ambalo linaendelea kumjengea mafanikio na ufanisi wa kazi zake katika wizara yake mhimu ambayo awali ilionekana kana kwamba asingelionekana kama mtendaji mzuri wa kazi.

ni jambo la kujivunia kwa kazi ambayo ameitenda kwa watanzania wote wanaendelea kumimina shukurani zao na pongezi kwa kwazi ambayo ameionyesha ya kishujaa,huyu ninayemzungumzia hapa ni waziri wa mifugo na uvuvi John Pmbe Magufuli,ama waweza kumwita shujaa anayepigania taifa katika kuhakikisha mali ya Tanzania haiibiwi kizembe.

Magufuli hivi karibuni alionyesha uwezo mkubwa na umakini baada ya kuikamata meli ya iliyosheheni mali kubwa yaani samaki ambao wamevuliwa na mataifa mbalimbali kama waphilipino,wachina na hata jirani zertu wake wamo.

umakini huu umepokewa kwa furaha na watanzania wote wapenda maendeleo shukurani zangu pia kama mtanzania zitamiminika kwa magufuli ambaye ni baba yetu wengine lakini swali lipo hapa? kama magufuli pekee ameweza kuwakamata hawa majangili na kuwaweka katika himaya yake kulikoni tunaendelea kupoteza muda wetu wa kuongelea mambo ya Dowans wakati huku tunawapa nafasi majangili kutuibia serikali inafanya hivyo kutufumba ili mali na haki ya Mtanzania iendelee kuibwa?.

kama ningelikuqwa kiongozi wa ngazi ya juu hii ingelikuwa kazi yangu ya kumpongeza kiongozi huyu ambye anafanya kazi kwa vitendo na sio kukaa ofisini akiwaagiza vibaraka waliopo chini yake.

Samaki ,dagaa,Papa,Sangara,Vibua na wengine wengi wametiwa katika nyavu za majangili sasa tutazamane katika sura zetu yup-i ameonyesha kusikitishwa na jambo hilo ambalo ni la kishujaa kwa Pombe magufuli?

Mawaziri wengine wanatakiwa kuiga vitu kama hivi na wakubaliane na ukweli kwamba magufuli ni kiongozi ambaye kila kukicha atakuwa bora kutokana na uwezo wake kikazi,tunashukuru kwa hilo maziwa yetu kwa hali hii yatakuwa salama, mfano ziwa Nyasa,kwa kina Nyasinta,Marcus Honors,Victoria kwa Ema kigolo, na mengine yakuwa salama bila kuwa na shaka.
kila jambo lina mwanzo na mwisho je akitoka magufuli nani ataweza kujitolea kama yeye?

Monday, March 2, 2009

Sunday, February 15, 2009

jesus

jana ilikuwa siku ya wapendanao lakini ajabu wengi walioneka kugombana katika kumbi mbalimbali iliniuma sana kuwaona wapenzi wakirushiana makopo ya bia ili hali walitoka nyumbani wamekumbatiana lakini walipofika bar au katika kumbi za starehe walioneka kutofautiana why? haya kazi ipo.

Saturday, February 14, 2009

dada wewe


wanasema kuwa....



Nakuuliza Je huyu Jamaa hapa nyuma ndiye naniiiiii au wewe unanicheka haya bwana

kumaliza


Mhhhh!

kuwepo kwa wingi wa vijana duniani ni challenge ya maisha kwa hiyo kaka yetu unatakiwa kuwa makini na kila jambo ambalo linaweza kuwa zuri ama baya vumilia kwa sababu unawengi wanaokutegemea huyo ni Maximo. uanashangaa ni hali hiyo tuliyonayo waTz

ok.


Unawajua hawa

inaweza kuwa!



Wasanii hawa ni maswahiba wanapendana sana na hapa ilikuwa siku ya uzinduzi wa killi Music Awards 2009. kulia ni LadyJaydeee Komandoo na kushoto kwake ni Keisha sauti ya Dhahabu utawapenda wakiimba kwa pamoja

panafaa kinoma hapo


Ebwanae ilikuwa ni siku ya uzinduzi wa kili music Award pale Bill Cannas kushoto ni mie katikati AY na kulia Betram asio.

Friday, January 23, 2009

Huyu si ngassa jamni ,kijana anaweza ile mbaya tumsifu na wakati nhuo huo tuendelee kuiwatengeneza kina Ngassa wengine

ukikaa hivyo hivyo napita kwa hiyo nakuja kaka si unanisikia kupitia wa cameroon sasa shangaa uone

aaah!


kuwepo kwa hawa wachezaji bado haitoshi kufika mbali zaidi ila tunawapongeza,kwa kazi kubwa ya uzeeni ili timu ya vijana vipi?

kivumbi Stars

pamoja na ukweli kuwa timu ya Taifa ya tanzania kuendelea kuteka hisia za mashabiki wengi wa soka hap nchini na nje ya nchi nyuma yake kuna maswali mengi ambayo wanasahau kuwa yapi maandalizi ambayo yanafanwa kuinusuru timu yetu isije ikaambulia patupu huko Ivary Coast ambako itashiriki kombe la Afrika kwa wachezaji wanaocheza ligi za ndani tu.

kuwepo kwa maswali hayo kunatokana na mambo mengi ambayo shirikisho la Soka la Tanzania TFF nilinaonyesha kuridhika na hatua ya timu ya Taifa ilivyo sasa ,akili yangu ilikuwa kama vile ndio safari ya kusajkata kabumbumbu inaanza kuiva lakini kwa upanende wa TFF wamekaa kimya kwani huu muda ulitakiwa timu hii iwe imesha fanya kazi kubwa zikiwepo mechi za kirafiki nyingi ili kuipa timu hiyo uzoefu mkubwa wa michuano hiyo ambayo si muda itaanza kutmua vumbi.

hiki ni kidokezo na changa moto kwa shirikisho la soka.

hizi nazo ziliwashika wa zamani unakumbuka



huyu ni msanii ambaye aliweza kupandikiza mbegu nzuri na salama ambapo amewaachia watoto urithi wa muziki Banana na Maunda je wewe baba yako alikuachaia kipi?.jibu unalo wewe.